Monday, September 7, 2015

Anonymous

LOVE YA UKWELI: MISS TZ AANZA SAFARI YA DUNIA KW STYLE HII!

Miss Tanzania 2014/15 Lilian Kamazima akitolewa damu kwaajili ya kuhamasisha jamii katika suala la uchangiaji damu safi na salama kwenye kituo cha Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam.
 
Kamazima akitolewa damu ndani ya Viwanja vya Mnazi mmoja.
 
Lilian akiwa ameshikilia damu hiyo muda mufupi baada ya kuhitimisha zoezi hilo la kuchangia damu safi na salama.
 
Mmoja wa wauguzi  katika kitengo cha damu safi na salama akiwa katika pozi na Miss Tanzania Lilian Kamazima muda mfupi baada ya kumaliza kutoa damu.
Na Musa Mateja
MISS Tanzania 2014/15 Lilian Kamazima jana aliweza kuchangia damu salama katika kituo cha Mnazi mmoja jijini Dar es Salaam, ikiwa ni moja ya huduma ya kuchangia jamii kabla ya kuanza safari yake ya kuelekea kwenye shindano la Miss World 2015 linalotarajiwa kufanyika nchini China hivi karibuni. 

Akizungumzia tukio hilo la kuchangia damu alisema kwamba, ameguswa na kuamua kutoa damu yake ili kuchangia baadhi ya Watanzania wenye matatizo na hasa ambao wamekuwa wakipoteza maisha yao kwakukosa damu safi na salama.
“Mimi kama miss Tanzania ni jukumu langu kuhakikisha nawahamasisha Watanzania wote kushiriki kwenye mambo ya kijamii mbalimbali likiwemo na hili la uchangiaji damu safi na salama, lakini kufanya hivyo pia ni moja mambo muhimu ambayo napaswa kuyafanya kabla siajaenda kuungana na warimbwende wenzangu mwezi wa kumi na moja tutakapokua kwenye mashindano hayo,” alisema Kamazima.
Habari/Picha: Musa Mateja/GPL.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.