Friday, September 4, 2015

Anonymous

Kikwazo Cha Wasanii Wa Tanzania ni Hiki...

Rapper Dogo Janja amesema kiu ya wasanii hapa nchini kwa serikali ijayo ni kuona wanapatiwa haki miliki ya kazi zao.
Dogo Janja
Dogo Janja ameiambia Bongo5 kuwa maisha mabaya kwa wasanii yamesababishwa na mfumo wa sanaa wa Tanzania ambao hauwanufaishi wasanii.
“Sioni kama ina maana kila mtu tumuulize wewe upo upande gani? Au wewe unamsapoti nani? Kila mtu ana haki ya kuchagua chama anachotaka. Kikwete kiukweli amecheza nafasi yake kwa wasanii, tuongee ukweli. Japo kuna mambo ya msingi bado kama sheria ya haki miliki,” amesema.
“Lakini haya tunayakabidhi kwa serikali ijayo. Sisi wasanii tatizo letu ni haki miliki. Shida ya wasanii ni haki miliki. Tukifanikiwa kupewa haki yetu kwa tunachofanya, basi wasanii tutafika mbali sana,” aliongeza rapper huyo.
-via Bongo5

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.