Na imelda mtema
Staa wa filamu Bongo, Kajala Masanja juzi kati aliangusha bonge ya
pati iliyogharimu takriban shilingi milioni saba ikiwa ni sehemu ya
kujipongeza kwa kazi ngumu ya ujaji aliyokuwa akiifanya kwenye shindano
la kusaka vipaji la Kinondoni (K.T.S) ambapo kwenye pati hiyo watu
walikunywa, kula na wengine walilewa kwa pombe kali.
Staa wa filamu Bongo, Kajala Masanja akiwakaribisha wageni waalikwa.
Akichonga na Ijumaa, Kajala alisema aliamua kufanya pati hiyo kwa
sababu kazi aliyokuwa nayo haikuwa rahisi lakini pia ilikuwa ni lazima
awapongeze washiriki wote walioingia fainali.“Nimeona nami nitumie fursa hii kuwapongeza washiriki wote waliongia kwenye fainali ya shindano hilo, pia ni muda muafaka wa kuongea nao mambo machache niliyoahidi kuwafanyia,” alisema Kajala.

Note: Only a member of this blog may post a comment.