Wednesday, September 9, 2015

Anonymous

ELEWA VYEMA KALENDA YA KUPATA MIMBA HAPA -2

Naendelea kuelezea kalenda ya kupata mimba ili ufahamu elimu hiyo.
Jambo lingine muhimu ni mwanamke kuchunguza idadi ya siku za mzunguko wake mrefu wa hedhi. Toa siku 11 kutoka katika idadi ya siku za mzunguko huo na utapata namba fulani.
Halafu tena anza kuhesabu katika mzunguko wako ujao wa hedhi kwenda mbele hadi kufikia siku ambayo una uwezekano wa kupata mimba. Kwa mfano iwapo mzunguko wako mrefu ni siku 31, toa 11 katika mzunguko huo na utapata 20.
Iwapo hedhi yako ijayo inaanza Oktoba 3, ongeza siku 20 kuanzia siku hiyo na Oktoba 23 itakuwa siku yako ambayo una uwezekano mkubwa wa kubeba mimba.
Kwa utaratibu huo utakuwa umepata kipindi cha kati ya Oktoba 14 hadi 23 ambacho ni siku ambazo una uwezekano mkubwa wa kubeba mimba au Ovulation window kitabibu.
Ovulation huweza kubadilika kidogo katika mzunguko wako wa hedhi kwa sababu Ovulation huweza kucheleweshwa na sababu mbalimbali kama vile wasiwasi au fikra nyingi, ugonjwa, lishe au kufanya mazoezi.
Kipindi cha Ovulation kinaainisha siku za kubeba mimba?
Kipindi cha kubeba mimba huanza siku 4 hadi 5 kabla ya Ovulation, na humalizika saa 24 hadi 48 hii ni kwa sababu muda wa Ovulation huweza kuchelewa au kuwahi kutokana na sababu mbalimbali. 

Pia kwa sababu mbegu ya kiume huwa na uhai kwa siku 4 hadi 5 na yai huweza kuishi kwa masaa 24 hadi 48 baada ya kuingia katika tumbo la uzazi. 

Hivyo kwa kujua siku hizo humsaidia mwanamke kufahamu kipindi chake cha Ovulation kimewadia na hivyo kuweza kukutana na mumewe au mwenza wake wakati huo ili aweze kubeba mimba.

Mambo ya kufanya ili kupata ujauzito haraka 

Leo tunaangalia jambo la kufanya ili mwanamke aweze kupata mimba.

Mwanamke unapaswa kuufahamu mzunguko wako wa siku za mwezi vizuri.
Mzunguko wa siku zako za mwezi utakusaidia kufahamu ni siku gani yai lako linakuwa limepevuka.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.