Kesi inayomkabili askofu wa kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima jana ilipelekea chup* yake kuoneshwa mbele hakimu mkazi wa mahamaka ya Kisutu, Cyprian Mkeha.
Pamoja na nguo hiyo ya ndani, vitu vingine vilivyotolewa kwenye begi la Askofu Gwajima ni suruali mbili, soksi, makoti mawili, bastola aina ya Berretta na risasi 17, CD mbili, chaja ya simu, hati ya kusafiria, vitabu na leseni ya kumiliki silaha.
Hatua hiyo ilifikiwa mahakamani hapo baada afisa wa Polisi idara ya upelelezi alijitambulisha kwa jina la Sospeter kutoa ushahidi wa kina kuhusu kesi hiyo na kutaka kutambua mmiliki wa begi lilifikishwa mahakamani hapo.
Baada ya kusikiliza ushahidi huo na kuwapa nafasi upande wa mshatikiwa kuuliza maswali, Hakimu Mkeha aliahirisha kesi hiyo hadi Oktoba 6 mwaka huu.

Note: Only a member of this blog may post a comment.