Friday, September 11, 2015

Anonymous

Baracka De Prince Autema UTAMU wa Agness MASOGANGE! Afunguka Kihivi...!

agnesmasogangegerald1.jpgBoniphace Ngumije
Msanii wa muziki, Baracka Endrew ‘Baracka De Prince’ amefunguka kuwa kufuatia skendo iliyokuwa inamkabili ya kutoka kimahaba na Video Queen maarufu Afrika, Agness Gerald ‘Masogange’ ameamua kujiweka naye kando mdogomdogo ili kuepusha maneno kutoka kwa wambeya.
Baraka 
Akichonga na Ijumaa juzikati, Baracka alisema anajua watu wanahisi ‘anabanjuka’ na ‘mtoto’ huyo kutokana na ukaribu wao hivyo ameona ni vyema afanye liwezekanalo ili kuondoa mawazo hayo kwa watu.
“Kiukweli yule wala siyo demu wangu na kwa kuwa huwa sipendi manenomaneno yasiyokuwa na ukweli, nimeamua kupunguza ukaribu na Masogange na hata picha zake nyingi Instargram nimefuta na yeye nilimwambia afanye hivyo akakubali,” alisema Baracka.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.