Saturday, August 22, 2015

Anonymous

Tunakubali watu WAMETUCHOKA, tuna kazi kubwa ya kujijenga na kurudisha imani – Asema Lundenga

Mkurugenzi wa Lino International Agency ambao ni waandaaji wa Miss Tanzania, Hashimu Lundenga amesema kuwa baada ya Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kulifungulia shindano hilo, sasa wana kazi kubwa ya kurudisha imani kwa mashabiki na wadhamini.
misstz
“Sisi kama Lino International Agency Ltd tumepokea taarifa za kufunguliwa kwa mashindano ya Miss Tanzania kwa furaha sana, mashindano haya yalifungiwa kwa miaka miwili sasa kufunguliwa kwa mashindano haya baada ya miezi saba au nane ni jambo kubwa sanaa, hivyo tumekubaliana na BASATA na tumepewa kibali cha maandalizi ya awali tunajua tumepoteza nafasi nzuri kwa wadhamini hivyo itatupa kazi kubwa kidogo kujijenga na kurudisha imani kwa wadhamini wetu tena,” alisema Lundenga. 

Akiongea na East Africa Radio, Ludenga amekiri kuwa kutokana na kujihusisha na mashindano hayo kwa muda mrefu kuna uwezekano watu wanahitaji kuona mabadiliko, hivyo wanampango wa kuweka kamati mpya itakayokuwa na watu wapya.
“…Inawezekana watu wamechoka sababu sisi tupo katika mashindano haya kwa miaka ishirini iliyopita hivyo tunakubali watu wametuchoka hivyo sisi wawili watatu hatutakuwa mstari wa mbele katika kamati hizo bali tutakuwa na kamati mpya ambayo itakuwa na watu wapya, maana watu wametuchoka hivyo lazima waje watu wapya wenye mawazo mapya na ndiyo watakuwa mstari mbele, hiyo itatusaidia kujua tumekosea wapi.”
Chanzo: Eatv.tv

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.