Tuesday, August 18, 2015

Anonymous

Nashangaa Wasanii Wanawaza Siasa Kuliko Kuiokoa Sanaa ya Filamu Inayokufa – ROSE NDAUKA

Msanii wa filamu Rose Ndauka amesema alishangazwa kuona wasanii wengi wakijitokeza kugombea nafasi mbalimbali za uongozi wakati wameshindwa kuisimania tasnia ya filamu.
11426390_1664350193786456_1066062253_n
Ndauka ameiambia Bongo5 kuwa alitegemea kuona wasanii wakiwekeza nguvu zao ili kuboresha umoja wao. “Mimi kiukweli nilishangaa wasanii wote kugombea, sio tu mmoja wote. Lakini pale pale niliwapongeza kwa sababu walithubutu, kwa sababu ndani yao wameona wana vitu vya kuwafanyia watu wao,” alisema. 

“Kitu ambacho kilinishtua nadhani bado tasnia yetu ya filamu inayumba. Nilikuwa nategemea wasanii wengi wawekeze nguvu zao kwenye tasnia yetu ya filamu na kuibadilisha kuitoa sehemu moja na kuipeleka sehemu nyingine, hicho ndicho kitu ambacho nilikuwa nategemea mimi. Kwahiyo sikushtuka kwa nia mbaya, nilishituka kwa sababu nilikuwa na mawazo yangu binafsi kwamba kuna siku wasanii watajitokeza kwa wingi kwa pamoja na tukashikamana kuibadilisha hii tasnia,” aliongeza.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.