Sunday, August 2, 2015

Anonymous

MWANACCM ATOA MBINU HII KWA CHAMA CHAKE ILI KUSHINDA UCHAGUZI UJAO ILA SI KWA BAO LA MKONO!

Wanachama wa chama cha mapinduzi mkoani Shinyanga wametakiwa kuvunja makundi yao yaliyokuwepo katika kampeni ya kura za maoni na kuunganisha nguvu zao kuwa kitu kimoja hali itakayoweza kuleta ushindi katika uchaguzi mkuu ujao huku aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo Mh.Steven Masele akiibuka kidedea kwa kura 7900 dhidi ya wagombea wengine tisa waliobaki sawa na asilimia 81.8 na kutangazwa rasmi kuipeperusha bendera ya chama cha mapinduzi katika kinyang'anyiro cha uchaguzi mkuu ujao wa mwezi October mwaka huu.

Hayo yamesemwa na katibu mkuu wa CCM wilaya Shinyanga mjini Bw.Charles Sangulo wakati akitangaza rasmi matokeo ya kura za maoni jimboni humo na kudai kuwa mchakato huo ulikuwa mkali uliojaa kashkash nyingi na vuta nikuvute za hapa na pale lakini palipo na ushindani lazima apatikane mshindi huku Mh.Steven Masele akiibuka mshindi na kuendelea kutetea jimbo la Shinyanga mjini.

Nao baadhi ya wananchi wa jimbo la Shinyanga mjimi hawakusita kutoa maoni yao kuhusiana na mchakato mzima katika kura za maoni na mabo yalikua kama ifuatavyo.

Aidha baadhi ya wagombea wengine walioshindwa kupata nafasi katika kinyanganyiro hicho wamelazimika kukubaliana na matokeo hayo kwa shingo upande huku wakidai kuwa malalamiko yao juu ya rushwa iliyokuwa imetawala katika kinyang'anyiro hicho yamekwama kwa madai kuwa yamekosa ushahidi wa kutosha hali iliyosababisha kubadilika kwa hali halisi ya matokeo hayo.

Na kwa upande wake msimamizi wa uchaguzi kura za maoni CCM kata ya Shinyanga mjini amemtangaza rasmi Bw.Gulam Hafiz Mukadama kuwa mshindi wa kiti cha udiwani kwa kupata kura 182 dhidi ya mgombea mwengine katika kinyang'anyiro hicho.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.