Staa wa filamu, Wema Sepetu
Mwandishi Wetu
KUMEKUCHA! Hivyo ndivyo unavyoweza kusema kufuatia mtifuano kati ya mtangazaji maarufu wa televisheni, Maimartha Jesse na staa wa filamu, Wema Sepetu baada ya bifu la wawili hao kufika jeshi la polisi.
KUMEKUCHA! Hivyo ndivyo unavyoweza kusema kufuatia mtifuano kati ya mtangazaji maarufu wa televisheni, Maimartha Jesse na staa wa filamu, Wema Sepetu baada ya bifu la wawili hao kufika jeshi la polisi.
Akipiga stori na gazeti hili, Maimartha alisema Wema alikuwa na nia
ya kumdhalilisha kwani baada ya kumtafuta na polisi na kumkosa, waliamua
kumpigia simu na kumuita kituoni Kijitonyama (Mabatini) ambako
alisomewa mashtaka ya kumtukana Wema katika mtandao wa kijamii wa
Instagram.
Mtangazaji maarufu wa televisheni, Maimartha Jesse
“Yaani Wema alitaka kunidhalilisha ndiyo maana polisi walikuja kibao
kwenye gari lao hapa dukani kwangu na waliponikosa ndiyo wakanipigia
simu kwamba niende mwenyewe kituoni, nikaenda nikatoa maelezo yangu ila
sasa nitakula naye sahani moja kwani watu wake wanaendelea kunitukana
sana mtandaoni nami siwezi kukubali,” alisema Maimartha.

Note: Only a member of this blog may post a comment.