Tuesday, August 4, 2015

Anonymous

Kura za Maoni 2015: Vurugu Zaitikisa Nchi Kila Kona! Shuhudia Hapa...

VURUGU POLISI (3)
Issa Mnally na Makongoro Oging’
Zoezi la kura za maoni katika vyama mbalimbali vya siasa hususan Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuchagua watakaopeperusha bendera kwenye uchaguzi mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 25, mwaka huu limezusha vurugu nchini nzima.

Habari ambazo zimelifikia gazeti hili zinasema sehemu mbalimbali kama vile Kiteto, mkoani Manyara, jijini Dar es Salaam, mkoani Mara, Dodoma, Mtwara, Mbeya na Ruvuma wakati wa zoezi hilo kulikuwa na vurugu katika baadhi ya maeneo.
Jijini Dar watu watano wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), walinusurika kuuawa na wenzao kwa madai kwamba walikuwa wakimfanyia kampeni mtu ambaye hawakumtaka.
20150801023012ll
Tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki katika pori la katikati ya  Msongola na Mvuti nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam saa mbili usiku baada ya watu wasiojulikana kuwavamia wenzao waliokuwa katika pilikapilika za kujiandaa na kura za maoni za wawania ubunge na udiwani kwa upande wa CCM.

Akisimulia jinsi tukio hilo lilivyowakuta mmoja wa watu hao aliyeomba jina lake kuhifadhiwa kwa sababu za kiusalama alisema kuwa, wao walikuwa wakitokea Kata ya Zingiziwa Chanika ambako kulikuwa na mkutano wa mgombea wanayemuunga mkono (jina linahifadhiwa).
Alisema kuwa baada ya kutoka kwenye mkutano huo, walitangulia Mvuti ambako mgombea wao huyo alikuwa amepanga akutane na wapiga kura wake.
 h
“Si unajua mikutano kama hii tunatangulia kwanza wapambe ili kuweka mambo sawa na kuwafanya wale wanaosubiri wawe na imani ya ujio wa mgombea, tukachukua gari letu aina ya Noah na kuelekea huko tukiwa kumi na mbili.
“Tukiwa tunakaribia kufika tukapigiwa simu na mtu ambaye hatukumfahamu, akatueleza kuwa tugeuze turudi haraka sana kwani kuna wapambe wanakuja kutufanyia fujo.
IMG_9824“ Baada ya kupata taarifa hiyo tukaanza kugeuza gari lakini ghafla likaja gari likaziba njia,  watu walioshuka katika gari hilo wakaja na kututoa kwenye gari na kuanza kutupiga wakitumia minyororo, huku wengine wakivunja vioo vya gari letu na mmoja alikuwa na bastola.
 “Walitufanyia vitendo vya kinyama kwa sababu akina mama tuliokuwa nao waliwavua nguo za ndani na kuwafanyia vitendo vya udhalilishaji,” alisema kada huyo wa CCM.
VURUGU POLISI (4)
Naye Ditriki Fabiani mmoja wa waathirika hao alikuwa na haya ya kusema: “Kwa kweli tumepigwa sana bahati ni kuwa kuna wenzetu watatu waliruka na kukimbilia Kituo cha Polisi Mvuti kutoa taarifa. Wale jamaa siyo watu kwani hata gari letu licha ya kuvunja vioo walitoa upepo, wakatoweka.”

Alisema baada ya hapo walienda kwa mwenyekiti wa serekali ya mtaa ambaye aliwapigia simu polisi nao wakafika na wakapelekwa Kituo cha Polisi Sitakishari ambako waliandikisha maelezo.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kipolisi, Ilala SACP Lucas Mkondya alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na akasema kuwa mtu mmoja amekamatwa kuhusiana na vurugu hizo.
VURUGU POLISI (7)
Huko Kiteto, Manyara mwandishi wetu ameripoti kuwa Ofisi ya CCM ya Wilaya ililazimika kufungwa mwishoni mwa wiki baada ya kutokea vurugu kubwa kutokana na kile kilichodaiwa kuwa ni upendeleo wa baadhi ya wagombea.

Vijana kadhaa wenye asili ya Kimasai wanachama wa CCM walivamia ofisi hiyo kwa madai kuwa walikuwa wakikataliwa kupiga kura ya maoni mpaka wawe na kadi mbili, ya CCM na ya mpiga kura inayotolewa na tume ya uchaguzi.
Ilibidi polisi wafike na kuwakamata vijana hao waliodai kuwa hawakuwa na hatia kwa sababu wasimamizi wa kura walitaka kupindisha kanuni za chama.
VURUGU POLISI (9)
Vurugu zingine zilitokea Tarime, Mara kwa madai kuwa kuna baadhi ya wagombea wapambe wao walikuwa na kura ambazo zilipigwa tayari.
Waliohusishwa na tukio hilo na kukanusha kuhusika ni Gaudensia Kabaka na Nyambari Nyangwine.
VURUGU POLISI (11)
Hadi juzi baadhi ya walioshinda kura za maoni kwa upande wa CCM ni Peter Serukamba Jimbo la Kigoma Mjini, Jonister Mhagama wa Songea aliyepita bila kupingwa Jimbo la Peramiho, Philimen Mollel wa Jimbo la Arusha alikuwa anaongoza.
Nape Nnauye wa Jimbo la Mtama aliongoza na Dk. Harrison Mwakyembe aliongoza Kyela. Kinondoni Idd Azam aliongoza na Korogwe Mjini, Mary Chitanda alikuwa anaongoza.
Naibu Waziri wa Afya, Dk. Steven Kabwe alipita bila kupingwa Jimbo la Serengeti.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.