Staa mwenye mvuto mkubwa Bongo Movies, Yobunesh Yusuph ‘Batuli’
Imelda Mtema
POLE sana! Staa mwenye mvuto mkubwa Bongo Movies, Yobunesh Yusuph ‘Batuli’ amepata pigo kufuatia nyumba anayoishi Mbezi Beach jijini Dar kuungua moto na kuteketeza vitu vyote ndani, Risasi Jumatano lina mkasa wote.
POLE sana! Staa mwenye mvuto mkubwa Bongo Movies, Yobunesh Yusuph ‘Batuli’ amepata pigo kufuatia nyumba anayoishi Mbezi Beach jijini Dar kuungua moto na kuteketeza vitu vyote ndani, Risasi Jumatano lina mkasa wote.
Akizungumza na paparazi wetu juzi huku akilia kwa uchungu, Batuli
alisema tukio hilo lilitokea jioni ya Jumamosi iliyopita yeye akiwa
saluni kwa ajili ya kwenda kwenye Fainali za Tanzania Movie Talents
(TMT) zilizofanyika usiku huo.
Alisema alipatwa na mshtuko mkubwa baada ya kurejea nyumbani kwake na kukuta nyumba hiyo imeungua na vitu vyote vimeteketea.
Vitu vilivyoteketea ni nguo zote za familia, vyombo, viatu, sofa,
stuli, redio, tivii, deki, feni. Kifupi, Batuli alisema hakuna
kilichotoka salama.
Akiendelea
kuzungumzia tukio hilo, Batuli alisema kuwa alipoondoka nyumbani hapo
kwenda saluni aliwaacha wasichana wawili wa kazi sanjari na mtoto wake.
Alisema: “Wao walipoanza kuona moshi mwingi walikwenda kugonga
milango ya majirani lakini hawakupata msaada wa haraka mpaka moto huo
uliotokea chumbani ukaenda jikoni ambako kulikuwa na jiko la gesi na
kusababisha mlipuko mkubwa.
“Kwa kweli hakuna kitu ambacho kimetoka ndani. Kuanzia nguo na kila
kitu hakuna kilichoweza kuokolewa zaidi ya wadada wangu wa kazi na mtoto
wangu. Yaani siwezi hata kuzungumza, niko katika kipindi kigumu sana na
hapa nahitajika maombi ili niweze kuwa katika hali ya kawaida.”
Msanii huyo alisema kuwa kwa sasa yeye na familia yake wamepata
makazi ya muda (hakutaka kuyataja) akimshukuru staa wa Bongo Movies,
Wema Sepetu kwamba alimpa msaada mkubwa.

Note: Only a member of this blog may post a comment.