Wednesday, August 26, 2015

Anonymous

Hii Ndio ilani ya CCM Uchaguzi Mkuu 2015...Biti Limebadilishwa ila Wimbo ni Ule Ule!

Vipaumbele:
1. Elimu
2. Afya
3. Kilimo
4. Miundombinu
5. Utawala bora
6. Mawasiliano
Swali: Je, kwa takribani miaka 54 ya kuwa madarakani wametekeleza hayo kwa kiwango gani cha kuridhisha wananchi?!

Je, kwa sasa kuna miujiza gani watakayotumia kutekeleza ilani hiyo?
Ilani kuu ya uchaguzi 2005 na 2010: Kasi mpya, Ari Mpya na Nguvu Mpya iliishia wapi? Maisha bora kwa kila mtanzania yako wapi? Nadhani ccm wanawaona watanzania kama mazuzu hivi, maana wanabadilisha biti tu lakini wimbo ni uleule!

 By UNDENIABLE View Post
Nionavyo:

Watanzania tumekwama hapa:
1. Elimu bora, na sio bora elimu kama ccm wanavyofanya. CCM wamechezea sana elimu hapa nchini. Kila kitu kimeparanganyika, kuanzia divisheni faifu. Elimu bora ni 'multiplier effect'

2. Uchumi.
Hapa ndio chimbuko la kuchukiwa CCM, bahati mbaya hawana habari. Uchumi umekufa!

Quote By UNDENIABLE View Post
Na hapa ndipo ninapoona umakini wa Lowassa. Yeye anaona vipaumbele vyake vikuu ni

1. Elimu bora
2. Kutokomeza umaskini (kukuza uchumi kwa maneno mengine)
Source:Jamii Forums

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.