WAKIJIANDAA na michuano ya Kombe
la Kagame, Yanga wameamua kufanya mazoezi yao kwa kificho kikubwa
kwenye Uwanja wa Chuo cha Polisi, Kurasini jijini Dar es Salaam.
Timu hiyo, ilianza kufanya mazoezi yake kwa mara ya kwanza jana Jumanne ikitokea Uwanja wa Karume waliokuwa wanautumia awali kabla ya kuhama.
Championi Jumatano,
lilifika kwenye uwanja huo kwa ajili ya kuripoti taarifa za timu hiyo,
lakini lilishindwa kufanikiwa kuingia ndani baada ya kuzuiliwa getini na
maofisa wa polisi hao.
Akizungumza na Championi Jumatano, Ofisa Michezo wa Jeshi na Mkurugenzi Msaidizi wa Ulinzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Inspekta Mohammed Manyai, alisema kuwa Yanga wamewataka kumzuia mtu yeyote kuingia kwenye mazoezi hayo.
Akizungumza na Championi Jumatano, Ofisa Michezo wa Jeshi na Mkurugenzi Msaidizi wa Ulinzi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Inspekta Mohammed Manyai, alisema kuwa Yanga wamewataka kumzuia mtu yeyote kuingia kwenye mazoezi hayo.
Manyai alisema, kwa mujibu wa benchi la
ufundi la timu hilo chini ya Kocha Mkuu Mholanzi, Hans van Der Pluijm,
hivi sasa mazoezi wanayoyafanya ni ya kimbinu, hivyo hawataki
kuyaonyesha kwa watu kwa hofu ya wapinzani wao kujua wanachofanya.
“Kikubwa Yanga wamezuia mazoezi yao yasiangaliwe na watu kwa ajili ya kuwaongezea umakini wachezaji wao kwa hofu ya kelele za mashabiki, pia kuficha mbinu zao wanazozitumia hivi sasa,” alisema. Yanga wameanza mazoezi leo (jana) asubuhi wenyewe watakuwa wanapishana na timu ya Kombaini ya Majeshi kila siku uwanjani; kila moja ikijiandaa na michuano yake.
Championi lilishuhudia
ulinzi mkali ukiwa umeimarishwa kwenye kambi hiyo na kila mmoja
aliyekuwa anataka kuingia alikuwa akihojiwa na kama siyo mhusika alikuwa
akizuiwa.
“Yanga watakuwa wanaanza mazoezi saa 2:30 hadi saa 5:00 asubuhi mara baada ya timu ya Kombaini ya Majeshi kumaliza mazoezi yake saa 2:00, asubuhi ambayo inaanza saa 12:00 asubuhi. “Wanapishana tena jioni kwa Kombaini ya Majeshi kuanza saa 8:00 mchana na kumaliza saa 10:00, kabla ya Yanga kuingia uwanjani kuanza mazoezi hayo saa 10:30 jioni hadi saa 12:00 jioni kisha kurudi kambini kwao huko Baraza la Maaskofu nyuma ya uwanja huo,” alisema Manyai.
“Yanga watakuwa wanaanza mazoezi saa 2:30 hadi saa 5:00 asubuhi mara baada ya timu ya Kombaini ya Majeshi kumaliza mazoezi yake saa 2:00, asubuhi ambayo inaanza saa 12:00 asubuhi. “Wanapishana tena jioni kwa Kombaini ya Majeshi kuanza saa 8:00 mchana na kumaliza saa 10:00, kabla ya Yanga kuingia uwanjani kuanza mazoezi hayo saa 10:30 jioni hadi saa 12:00 jioni kisha kurudi kambini kwao huko Baraza la Maaskofu nyuma ya uwanja huo,” alisema Manyai.

Note: Only a member of this blog may post a comment.