Dayna Nyange amekiri kuwa cover la wimbo wake ‘Nitulize’ akiwa na Nay
wa Mitego lilimletea shida kutokana na kuchukuliwa na jamii kama sio
mtu wa aina hiyo.
Dayna ameiambia Bongo5 kuwa kama wazazi wake wangeona cover ya wimbo huo, wangejisikia vibaya kwakuwa ni watu wadini.
“Unajua muziki unatufanya tufanye vitu fulani kwaajili ya muziki na
mashabiki wetu. Lakini tunaporudi kwenye maisha ya kawaida mimi ni mtu
mwenye kujali maadili,” amesema Dayna.
“Sema kwenye issue ya cover ya wimbo ‘Nitulize’ iliniletea shida kwa
baadhi ya watu na nafikiri zile picha zingewafika wazazi wangu ingekuwa
tatizo kidogo, lakini ndo hivyo sio watu wa kwenye social network. Pia
mimi ni mtoto wa kiislamu lazima nizingatie kujistili kwenye kazi zangu.
Hata ujio wa video yangu utazingatia masuala ya kujistili,” aliongeza
Dayna.
Amesema video ya wimbo huo itatoka baada ya mwezi wa Ramadhan.
-via bongo5

Note: Only a member of this blog may post a comment.