Mwigizaji wa filamu za Kibongo, zao la Kundi la Kaole, Nuru Nassoro ‘Nora’.
Brighton Masalu
Mwigizaji wa
filamu za Kibongo, zao la Kundi la Kaole, Nuru Nassoro ‘Nora’ amesema
kwa sasa hafikirii tena kuingia kwenye uhusiano wa mapenzi na kwamba
anaamua kuelekeza nguvu na akili zote kwenye kazi.
Nora ameliambia Amani kwamba, ameamua kuwa hivyo baada ya kuambulia maumivu mara nyingi katika mapenzi, jambo ambalo limechangia kumdidimiza kisanii.
“Sitaki tena kusikia habari za mapenzi, kwa sasa naelekeza nguvu zote kwenye kazi tu,” alisema Nora.

Note: Only a member of this blog may post a comment.