Thursday, July 30, 2015

Anonymous

SIMBA SC Watamrudisha JUMA KASEJA Kweli? Majibu ya Uhakika Yapo Hapa

Simba kwa hivi karibuni imeonekana kufanya usajili kwa usiri zaidi, huwezi kusikia fununu za kutangaza kumuhitaji fulani hadi uhamisho ukamilike, Simba imerejesha baadhi ya wachezaji wake wakongwe kikosini kama Musa Hassan Mgosi na Mwinyi Kazimoto hivyo baada ya klabu hiyo kutangaza kuhitaji golikipa mmoja aongeze nguvu kikosini, zilizuka tetesi za kutaka kurejeshwa kwa Juma Kaseja.
juma-kaseja
Juma Kaseja ni moja kati ya wachezaji waliowahi kuichezea Simba kwa mafanikio, kabla ya kuhamia Yanga, Kaseja ambaye ni mchezaji huru baada ya kuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu zilikuwwepo fununu za baadhi ya viongozi wa Simba kumpeleka Oman akajifue ili aje ajiunge na Simba.
KasejaJuma
Lakini pia zilikuwepo fununu za mgawanyiko wa viongozi klabuni, wapo wanaoafiki Kaseja Kurudi na wapo ambao hawamtaki Kaseja, team ya millardayo.com ilibidi kumtafuta mkuu wa idara ya habari ya Simba Haji Manara kuweka sawa suala hilo.
JumaKaseja1AFROKIJABLOGGER
“Kaseja kurudi maana yake nini, Kaseja kurudi hakuna ulazima wa hilo maana yake tukisema tumrudishe Kaseja itabidi tumrudishe na Mwameja tumrudishe Idd Pazi aje kudaka tumrudishe kila mtu sasa kila zama zinagolikipa wake mimi sidhani kama hata huo mvutano  wa nini sasa huo mvutano Kaseja alikuwa mchezaji wa Simba nadhani labda atakapo hitajika arudi atarudi” >>>Manara
“lakini kwa hivi sasa hatumzungumzii Juma Kaseja tunayo mipango mingine itakapofika kama mfano  benchi la ufundi likasema linamuhitaji Kaseja tutalizungumzia right now hatuna mpango na Juma Kaseja”>>> Manara

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.