Brighton Masalu
Mwigizaji wa kitambo Bongo, Ruth Suka
‘Mainda’ amesema kutokana na muonekano wake wa ‘usiriaz’, imekuwa ni
kinga imara inayosababisha kukimbiwa na wanaume wakware.
Akizungumza na Amani, Mainda aliyewahi
kuripotiwa kutoka na mwigizaji Vincent Kigosi ‘Ray’ alisema wakati
mwingine wanaume huangalia ‘hali ya hewa’ kwa mwanamke kabla ya kumfuata
na kumueleza mambo ya uhusiano.
“Unajua usiriaz wangu huu unaniepushia
mambo mengi sana, wanaume wananikimbia na wananiogopa mno, hata kama
siyo mkorofi lakini wanajiuliza huyu nitamuingiaje?” alisema Mainda.

Note: Only a member of this blog may post a comment.