Wednesday, March 25, 2015

Anonymous

INATISHA SANA! MSICHANA AMUUA MPENZI WAKE KISA NDOTO!

bloody_hands
Mwanamke mmoja nchini Nigeria anashikiliwa na Polisi kutokana na kosa la mauaji ya mtu ambaye alikuwa ni mpenzi wake.. kisa chote kilianzia kwenye ndoto !! 

Mwanamke huyo Monsurat Yusuf alishtuka toka usingizini na kumsimulia mpenzi wake, Eric Moses kwamba ameota ndoto ambayo alihisi amepigwa na mpenzi wake huyo makofi akiwa usingizini. 

Eric alicheka baada ya kusikia story hiyo lakini kumbe Monsurat hakupenda, akachukua kisu na kumchoma mpenzi wake huyo ambaye alifariki.
Upelelezi wa Polisi umeonesha wote wawili walikuwa ni wanafunzi na walikuwa wakiimba kwaya pia ya kanisa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.