Wednesday, July 15, 2015

Anonymous

Nikki wa Pili ataja sababu za Lord Eyez kutosikika kwenye kazi za Weusi kwa kipindi kirefu!

Ni kipindi kirefu rapper Lord Eyez hajasikika katika kazi za wasanii wenzake wa kundi la Weusi, wala hajatoa kazi zake binafsi.
WEUSI_full
Miezi michache iliyopita Nikki wa pili alitoa wimbo wa ‘Safari’ aliowashirikisha members wa Weusi akiwemo Joh Makini na G-Nako, baadae Joh akatoa ‘Nusu Nusu’ aliyomshirikisha G-Nako, G-Nako naye alitoa ngoma aliyomshirikisha Joh, lakini rapper Lord Eyez hajahusika wala kutoa ngoma zake binafsi kwa kipindi kirefu.
Msemaji wa Weusi, Nikki Wa Pili ameiambia Bongo 5 kuwa Lord Eyes bado ni member wa kundi hilo, lakini ratiba zake binafsi zinazomfanya awe Arusha muda mrefu ndio zimepelekea kutoshiriki kwenye kazi za members wa Weusi ambazo mara nyingi hufanyika Dar. 

“Lord Eyez yuko kwenye kundi lakini unajua sisi ni kampuni halafu inategemeana na ratiba zako binafsi.” Alisema Nikki wa Pili. “Kwa mfano ukimwangalia Bonta yuko Kahama kwahiyo namna yake ya kurekodi inategemeana na kazi yake, Lord Eyez kwa kipindi kirefu sana amekuwa yuko Arusha. Kwahiyo ana kazi zake anafanya, unajuwa kila mtu anafanya kazi zake hata mimi nafanya kazi zangu na ukiangalia huu mwaka kuanzia umeanza mpaka saizi hatujafanya kazi ya kundi ambayo imetoka, kwahiyo imekuwa hizi kazi za kila mtu anafanya binafsi.” 

Nikki ameelezea jinsi members wa Weusi hufanya kazi zao;
“Huu ufanyaji kazi binafsi inategemea na mazingira na uko wapi, kwa mfano kwa ‘Safari’ sio kwamba nilipanga kufanya na kina Joh, ni kwamba walikuwepo wakati kazi inafanyika Lord Eyez hakuwepo kwahiyo labda angekuwepo labda angeweza kuwepo. G-Nako nyimbo yake mpya ambayo amenishirikisha nilikuwepo wakati anafanya, na unajua sisi hatuna rules…” 

“Lord Eyez saizi ni kama miezi nane hivi yuko Arusha, na sisi kazi nyingi tumefanya huku (Dar) kwahiyo ndo maana labda amekuwa hajaonekana sasna kwenye kazi za mmoja mmoja ambazo zimetoka lakini kazi zake anazo. Tunasubiri yeye mwenyewe asema anataka kutoa lini kila mtu ana ratiba yake binafsi, kwahiyo unapokuwa umejipanga then unawasilisha kwenye kundi jamani mi kazi yangu nafanya hivi then sisi kama member tuna support kama tunavyo sapotiana.” Alimaliza Nikki Wa Pili.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.