Friday, July 3, 2015

Anonymous

MWADUI FC Balaa! Yawafuata MKUDE, NGASSA Sauz!

Kiungo wa Simba, Jonas Mkude.
Martha Mboma, Dar es Salaam
WAKATI ikiendelea kujifua kwa ajili ya msimu ujao katika kambi yao iliyopo ndani ya mgodi wa Mwadui, Mwadui FC imedaiwa kuwa ina mpango wa kwenda Afrika Kusini ‘Sauz’ kujiandaa zaidi

Katibu wa klabu hiyo, Ramadhan Kilao, ameliambia gazeti hili kuwa, mpango huo upo ikiwa na maana kuwa watakwenda katika nchi hiyo ambapo ndipo alipo kiungo wa Simba, Jonas Mkude ambaye yupo kwenye majaribio ya kucheza soka la kulipwa katika timu ya Bidvest Wits inayoshiriki Ligi Kuu ya Sauz.

“Tunafanya maandalizi yetu hapa kwa sasa lakini mpango mzima mambo yakiwa sawa muda wowote tunatarajia kwenda Sauz, wachezaji wote wapo tayari isipokuwa mmoja tu ndiyo kafiwa na mama yake,” alisema kiongozi huyo ambaye timu yake inanolewa na Kocha Jamhuri Kihwelo ‘Julio’.

Ikiwa itakuwa hivyo, Mwadui itakuwa imeonyesha umwamba kwa timu iliyopanda daraja kwenda mpaka Sauz kwa ajili ya kujiandaa na msimu, jambo ambalo ni nadra kutokea kwenye soka la Tanzania.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.