Gladness mallya BAADA
ya mwanamuziki wa Dansi nchini, Ramadhan Masanja ‘Banza Stone’ kulazwa
katika Hospitali ya Mwananyamala, Dar kwa siku saba, hatimaye
ameruhusiwa kurejea nyumbani baada ya kupata nafuu.
“Tunamshukuru Mungu mgonjwa wetu ameruhusiwa japo bado hali yake haijatengamaa kwani tofauti na matatizo ya awali ya fangasi za kichwani, anakabiliwa na upungufu wa damu hivyo tumeshauriwa tumpe vyakula vya kuongeza damu,” alisema Hamis.

Note: Only a member of this blog may post a comment.