Mbunge wa jimbo la Mpanda Mjini kwa miongo miwili, Said Amour Alfi (CHADEMA) amejiunga rasmi na CCM. Amekuwa miongoni mwa makada 23 wa chama hicho, waliochukua na kurejesha fomu za kuomba kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25, mwaka huu.
Arfi amechukua fomu kuwania ubunge katika jimbo jipya la Nsimbo, wilayani Mlele. Mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, chini ya uongozi wa Freeman Mbowe, alitangaza kujivua uanachama wake Chadema hivi karibuni katika mkutano wa hadhara katika uwanja wa Shule ya Msingi Kashaulili mjini Mpanda, huku akisisitiza kuwa alikotoka alichoshwa na siasa za kinafiki.
Katibu wa CCM wa Mkoa wa Katavi, Averin Mushi amethibitisha kuwa Arfi alichukua na kurejesha fomu za maombi ya kugombea ubunge katika jimbo jipya la uchaguzi la Nsimbo kwa tiketi ya CCM .
Hivi karibuni , Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza majimbo mapya ya uchaguzi, ambapo Jimbo la Katavi limegawanywa na kuanzishwa kwa majimbo mawili ya Uchaguzi ya Nsimbo na Kavuu.
Akitangaza idadi ya makada wa CCM waliorejesha fomu za kuomba kugombea ubunge katika majimbo manne ya uchaguzi mkoani humo, Mushi alieleza kuwa hadi pazia lilipokuwa likifungwa Jumapili, makada 23 wa chama hicho, akiwemo Arfi, walikuwa wamerejesha fomu zao .
Alisema kuwa katika Jimbo la Nsimbo makada waliorejesha fomu ni pamoja na Arfi, Shaaban Hassanali “Dallah”, Richard Mbogo, Manamba Emmanuel na Mapesa Frank.
Alitaja makada waliorejesha fomu jimbo la Katavi kuwa ni Isaack Kamwele, Meneja wa Tanroads mkoa wa Katavi na Shafi Mpenda ambaye ni Mhasibu wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN) inayochapisha gazeti hili na magazeti dada ya Daily News, Sunday News, HabariLeo Jumapili na SpotiLeo.
Wengine ni Maganga Kampala na Oscar Albano. Alisema katika jimbo jipya la Kavuu, waliorejesha fomu ni Zumba Emmanuel Mselem, Abdallah Saida ambaye ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Katavi na Prudencia Kikwembe, Mbunge Viti Maalumu.
Arfi aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa, kabla ya kujiuzulu wadhifa huo na baadaye kujivua uanachama hivi karibuni aliwahi kutuhumiwa na Chadema kumsaidia Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kupita bila kupingwa katika Jimbo la Katavi (CCM) kwa Uchaguzi Mkuu wa 2010 kwa kuwashawishi baadhi ya wagombea kuondoa majina yao.
Hata hivyo, Arfi amekuwa akikanusha tuhuma hizo na kusababisha kutokuelewana na baadhi ya viongozi wenzake ambapo alifikia uamuzi wa kujiuzulu nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa Novemba 22, mwaka 2013 kwa kile alichosema amechoshwa na siasa za kinafiki ndani ya chama hicho.
Aidha, katika waraka wake wa kujiuzulu Umakamu Mwenyekiti, alisema hakuwa tayari kubanwa na hata kuchaguliwa aina ya marafiki. Sehemu ya waraka huo inasomeka.
Arfi amechukua fomu kuwania ubunge katika jimbo jipya la Nsimbo, wilayani Mlele. Mwanasiasa huyo aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Taifa wa Chadema, chini ya uongozi wa Freeman Mbowe, alitangaza kujivua uanachama wake Chadema hivi karibuni katika mkutano wa hadhara katika uwanja wa Shule ya Msingi Kashaulili mjini Mpanda, huku akisisitiza kuwa alikotoka alichoshwa na siasa za kinafiki.
Katibu wa CCM wa Mkoa wa Katavi, Averin Mushi amethibitisha kuwa Arfi alichukua na kurejesha fomu za maombi ya kugombea ubunge katika jimbo jipya la uchaguzi la Nsimbo kwa tiketi ya CCM .
Hivi karibuni , Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) ilitangaza majimbo mapya ya uchaguzi, ambapo Jimbo la Katavi limegawanywa na kuanzishwa kwa majimbo mawili ya Uchaguzi ya Nsimbo na Kavuu.
Akitangaza idadi ya makada wa CCM waliorejesha fomu za kuomba kugombea ubunge katika majimbo manne ya uchaguzi mkoani humo, Mushi alieleza kuwa hadi pazia lilipokuwa likifungwa Jumapili, makada 23 wa chama hicho, akiwemo Arfi, walikuwa wamerejesha fomu zao .
Alisema kuwa katika Jimbo la Nsimbo makada waliorejesha fomu ni pamoja na Arfi, Shaaban Hassanali “Dallah”, Richard Mbogo, Manamba Emmanuel na Mapesa Frank.
Alitaja makada waliorejesha fomu jimbo la Katavi kuwa ni Isaack Kamwele, Meneja wa Tanroads mkoa wa Katavi na Shafi Mpenda ambaye ni Mhasibu wa kampuni ya magazeti ya Serikali (TSN) inayochapisha gazeti hili na magazeti dada ya Daily News, Sunday News, HabariLeo Jumapili na SpotiLeo.
Wengine ni Maganga Kampala na Oscar Albano. Alisema katika jimbo jipya la Kavuu, waliorejesha fomu ni Zumba Emmanuel Mselem, Abdallah Saida ambaye ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Katavi na Prudencia Kikwembe, Mbunge Viti Maalumu.
Arfi aliyewahi kuwa Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa, kabla ya kujiuzulu wadhifa huo na baadaye kujivua uanachama hivi karibuni aliwahi kutuhumiwa na Chadema kumsaidia Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kupita bila kupingwa katika Jimbo la Katavi (CCM) kwa Uchaguzi Mkuu wa 2010 kwa kuwashawishi baadhi ya wagombea kuondoa majina yao.
Hata hivyo, Arfi amekuwa akikanusha tuhuma hizo na kusababisha kutokuelewana na baadhi ya viongozi wenzake ambapo alifikia uamuzi wa kujiuzulu nafasi ya Makamu Mwenyekiti wa Chadema Taifa Novemba 22, mwaka 2013 kwa kile alichosema amechoshwa na siasa za kinafiki ndani ya chama hicho.
Aidha, katika waraka wake wa kujiuzulu Umakamu Mwenyekiti, alisema hakuwa tayari kubanwa na hata kuchaguliwa aina ya marafiki. Sehemu ya waraka huo inasomeka.
Note: Only a member of this blog may post a comment.