Hatimaye jina la katibu Mkuu wa Chadema Dk Wibroad Slaa limeteuliwa na UKAWA kuwa mgombea wake wa nafasi ya Urais katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba.
Baadhi ya wajumbe wa kamati maalumu inayoongozwa na viongozi wa kitaifa jana walithibitisha kuteuliwa kwa Slaa kwa kueleza kuwa tayari jina lake limeshapitishwa na linatarajiwa kutangazwa rasmi baada ya kumalizika kwa kikao cha kamati hiyo.
Aidha walieleza kuwa watatangaza wagombea wenza.
Ibrahim Lipumba ambaye awali alitangaza kuitaka nafasi hiyo, atautumia mkutano huo baina ya viongozi wa Ukawa kuliondoa jina lake ili kumpisha Slaa kugombea ili kulinda maslahi mapana na mafanikio ya Umoja huo.

Note: Only a member of this blog may post a comment.