Friday, July 3, 2015

Anonymous

INATISHA! Auawa Kikatili Kwa Kutenganishwa Kichwa na Mwili Kisha Kichwa Chahifadhiwa Kwenye Mfuko Huko Tanga

Kikongwe Yohana Msumari anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 80, ameuawa kikatili kwa kutenganishwa mwili na kichwa na kisha wauaji hao kukihifadhi kichwa hicho kwenye mfuko wa plastiki chini ya mwembe. 

Hata hivyo mtu anayesadikiwa kufanya mauaji hayo, alisakwa na wananchi wenye hasira na kisha kukamatwa na kuonesha mwili wa marehemu huyo na yeye kupigwa na hatimaye kuuawa pia. 

Tukio hilo la kusikitisha lilitokea juzi, katika kijiji cha Mamboleo, Kata ya Bwembwera wilayani Muheza mkoani Tanga, ambapo kikongwe huyo aliondoka na kijana ambaye naye hakutambulika jina lake mwenye umri wa kati ya miaka 35-40 wa kabila la Kinyaturu, ambaye alikuwa mfanyakazi za vibarua kwenye mashamba ya watu. 

Akisimulia tukio hilo, Katibu Kata wa Chama Cha Mapinduzi kwenye Kata ya Bwembwera, Achi Semhando alisema tukio hilo la kusikitisha lilitokea kwenye kata yao na kwamba polisi walifika baada ya kupewa taarifa hizo na kuchukia maiti.
“Kwa kweli ni tukio la kusikitisha, huyu mzee aliondoka na huyo kijana na kwenda kumuonesha sehemu ya kufyeka shambani kwake, ila hadi jioni huyu mzee hakurudi na ndipo wananchi waliingiwa na wasiwasi na kuamua kumtafuta huyo kijana aliyeondoka naye,” Semhando. 

Kijana huyo alipatikana na wananchi walimtaka aseme mzee huyo alipo na ndipo aliwapeleka hadi shambani na kuona maiti ya mzee huyo na ndipo walianza kumpiga hadi umauti wake na kisha kutoa taarifa polisi. 

Hata hivyo maiti ya mzee huyo haikuwa na kichwa na polisi walizichukua maiti zote mbili na kwamba ilipofika jana asubuhi, watoto waliokuwa wakiokota maembe kwenye miti waliona mfuko umefungwa na walipouchunguza waliona kichwa na kutoa taarifa kijijini.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.