Friday, July 3, 2015

Anonymous

MIZENGO PINDA Afunguka Kuhusu FITINA Uchguzi Mkuu 2015

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, amelezea hofu yake juu ya kuwapo kwa fitina zinazofanywa na baadhi ya watu kwa nia ya kuwaharibia wengine katika mchakato unaoendelea wa makada 42 wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanaowania kuteuliwa kugombea nafasi ya urais kupitia chama hicho. 
Pinda ambaye pia ni mmoja wa makada waliochukua fomu kutaka kuteuliwa kuwa wagombea wa urais wa CCM, alisema namna pekee ya kuwaepuka watu wanaofitinisha wenzao ni kutowaunga mkono. 

Aidha, Pinda aliwataka pia watangaza nia wenzake watakaoshindwa katika kinyang’anyiro hicho kukubali matokeo na kumuunga mkono yeyote atayeibuka mshindi na pia kutambua kuwa ‘asiyekubali kushindwa si mshindani’.
Pinda aliyasema hayo wakati akihutubia kwenye viwanja vya Mashujaa mjini hapa wakati akifunga sherehe za maadhimisho ya wiki ya Serikali za Mitaa. 

Alisisitiza umuhimu wa kuendelea kuwapo kwa amani na utulivu nchini hata baada ya uchaguzi kumalizika, huku akiwaasa wanasiasa wote kujiepusha na vitendo vya fujo kwani hazina tija kwa taifa na kwamba siasa ni ushindani ambao kila mtu anatakiwa akubaliane na matokeo.
“Acheni kuweka chuki zisizo na tija, haitowasaidia. Acheni kutaka kuwafanyia fujo wale watakaokuwa wamekubalika katika ngazi mbalimbali kutuongoza, maana wengine kazi yao ni fitina tu na wanataka mambo yaende ovyo. Mzalendo wa kweli ni yule anayekubali, kama kura hazikutosha hazikutosha tu,”. 

Alitoa wito pia kwa wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kuhakikisha kuwa wanasimamia vizuri uchaguzi mkuu pale mchakato utakapoanza. “Agizo langu kwa wakurugenzi, tunakwenda katika uchaguzi mkuu. Tusifanye mzaha na chaguzi hizi, hakikisheni mnasimamia vizuri kama sheria zinavyoelekeza na kama kanuni zinavyoelekeza,” aliongeza. 

Mwenyekiti wa Jumuia ya Umoja wa Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT) na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Didas Masaburi, alisema baadhi ya halmashauri nchini zimefanikiwa kupunguza tatizo la uhaba wa madawati kwa zaidi ya asilimia 80.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.