Thursday, July 2, 2015

Anonymous

ESTER WA BONGO MUVI AZIDI KUTESWA NA TUMBO LA BIA!

Brighton Masalu  
KUNENEPEANA! Kuvimbiana na kuongezeka kwa ukubwa wa tumbo kunazidi kumpa wakati mgumu msanii ‘anayechungulia’ katika gemu la uigizaji, Ester Kiama kufuatia kusongwa na madai kuwa ‘amebugia kijusi’ (mjamzito) huku Kulwa Kikumba ‘Dude’ akidaiwa kuwa baba kijacho.

Msanii ‘anayechungulia’ katika gemu la uigizaji, Ester Kiama.
Akikutanisha ‘lips’ na paparazi wetu hivi karibuni, Ester alisema licha ya kuwaeleza watu kwamba ukubwa wa tumbo lake unatokana na utumiaji wa vinywaji vyenye ngano (kama bia) na uvivu wa kufanya mazoezi, lakini wao wamekuwa wakimkomalia kuwa ni mimba.
“Watu wengi wanasema nina mimba. Wengine wanakwenda mbele zaidi wakinipongeza kwa kumbebea mimba Dude. Yaani napata wakati mgumu,” alisema Ester.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.