Imelda mtema
Makubwa! Lile kalio la haja la muuza nyago maarufu kwenye
video za wasanii wa Bongo Fleva, Agness Gerald ‘Masogange’ limesababisha
ajali kati ya bodaboda na Bajaj maeneo ya Sinza-Mori baada ya mrembo
huyo kushuka kwenye gari akielekea saluni.
“Yaani aliposhuka Masogange tu kwenye gari yule mwendesha bodaboda hakuwa anaangalia mbele kabisa wakati Bajaj ilikuwa ikija kwa kasi hivyo akashindwa kuikwepa akaivaa na kumrusha dereva wa bodaboda upande mwingine kwa kishindo,” alisema shuhuda.
Mpashaji wetu alizidi kuweka wazi kuwa baada ya ajali hiyo kutokea, watu walikusanyika kitendo ambacho hata Masogange kilimshtua na kumfanya asimame kuangali tukio hilo.
Hata hivyo, shuhuda huyo alisema madereva hao walielewana na kuyamaliza palepale.
Baada ya gazeti hili kupata ‘ubuyu’ huo, lilimtafuta Masogange ambapo alikiri kutokea kwa ajali hiyo lakini mwanzo hakujua kama yeye alikuwa chanzo cha ajali hiyo.
“Unajua mimi nilivyosikia kishindo na watu wakipiga makelele sikujua kama nilikuwa chanzo hadi niliposikia watu wanaanza kunong’ona maana hata mimi nilikuwa nashangaa na kujikuta nikicheka tu kwani sikujua wowowo langu lilisababisha shida,” alisema.

Note: Only a member of this blog may post a comment.