Wanafunzi wa chuo kikuu cha Garissa wakitoroka shambulio
Serikali
ya Kenya imemtambua mmoja ya wapiganaji waliohusika katika mauaji ya
chuo kikuu cha Garissa kwamba ni mtoto wa afisa wa serikali.Msemaji wa wizara ya ndani amesema kuwa Abdirahim Abdullahi ni miongoni mwa watu wanne walioshambulia chuo kikuu cha Garissa siku ya alhamisi na kuwaua watu 148.
Mtu huyo sasa ametambulika kama mwana wa kiume wa Chifu wa eneo la Kazkazini mashariki mwa Kenya. Alidaiwa kutoweka na ilihofiwa kwamba amesafiri nchini Somalia.
Wizara ya ndani inasema kuwa wapiganaji wote waliuawa siku ya alhamisi. Washukiwa wengine watano wamekamatwa kufikia sasa kwa kuhusishwa na mauaji hayo ambayo ni mabaya zaidi kuwahi kutekelezwa na kundi la wapiganaji wa Alshabaab.


Note: Only a member of this blog may post a comment.