Mwenyekiti wa CHADEMA taifa Bw. Freeman Mbowe.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa chama hicho wa ngazi ya shina hadi wilaya wa mkoa wa Dar es salaam, mwenyekiti wa Chadema taifa Bw. Freeman Mbowe ameitaka serikali kuharakisha zoezi la uandikishaji wapiga kura na kusisitiza tarehe ya kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu ilijulikana nchi nzima kutokana kuwepo kikatiba na kisheria kuwa ni jumapili ya mwisho wa mwezi wa 10.
Awali wakizungumza na mamia ya viongozi wa chama hicho katika mkutano huo naibu katibu mkuu wa chadema Zanzibar Bwana Salum Mwalimu amesema lengo la chama hicho kuwa na viongozi wenye weledi na uwezo wa kufanya kazi,huku naibu katibu mkuu wa chama hicho Tanzania bara Mhe. John Mnyika amesema mafunzo hayo yataendeshwa nchi nzima ambapo yanatarajiwa kuwafikia viongozi wa chama zaidi ya laki 2 na ishirini na nne elfu.

Note: Only a member of this blog may post a comment.