Friday, April 17, 2015

Anonymous

MBOWE AILIPUA SERIKALI!

Mwenyekiti wa CHADEMA taifa Bw. Freeman Mbowe.
Chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA kimedai kuwa hakitakubali serikali ya awamu ya nne kuongezewa muda wa kukaa madarakani kutokana na kusuasua kwa zoezi la uandikishwaji wa daftari la wapiga kura.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa mafunzo ya kuwajengea uwezo viongozi wa chama hicho wa ngazi ya shina hadi wilaya wa mkoa wa Dar es salaam, mwenyekiti wa Chadema taifa Bw. Freeman Mbowe ameitaka serikali kuharakisha zoezi la uandikishaji wapiga kura na kusisitiza tarehe ya kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu ilijulikana nchi nzima kutokana kuwepo kikatiba na kisheria kuwa ni jumapili ya mwisho wa mwezi wa 10. 

Awali wakizungumza na mamia ya viongozi wa chama hicho katika mkutano huo naibu katibu mkuu wa chadema Zanzibar Bwana Salum Mwalimu amesema lengo la chama hicho kuwa na viongozi wenye weledi na uwezo wa kufanya kazi,huku naibu katibu mkuu wa chama hicho Tanzania bara Mhe. John Mnyika amesema mafunzo hayo yataendeshwa nchi nzima ambapo yanatarajiwa kuwafikia viongozi wa chama zaidi ya laki 2 na ishirini na nne elfu.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.