MAHAKAMA nchini Misri inatarajia kutoa hukumu kwenye kesi kadhaa
zinazomkabili rais wa zamani, Mohammed Morsi ambaye aliondolewa
madarakani na jeshi mwaka 2013.
Mosri anakabiliwa na kesi pamoja na viongozi wengine wa Kundi la Muslim Brotherhood kwa kuwachochea wafuasi kumuua mwandishi wa habari na waandamanaji wa upinzani wakati wa makabiliano nje ya ikulu ya rais mwaka 2012.
Mawakili wanaomtetea Mosri wanasema kuwa huenda akakabiliwa na hukumu ya kifo. Mamia ya wafuasi wa Kundi la Muslim Brotherhood wamehukumiwa kifo katika mikakati ya kukabiliana na kundi hilo lililopigwa marufuku na rais wa sasa Abdul Fattah al-Sisi.
Kundi la Muslim Brotherhood limemlaumu rais kwa kutumia mahakama kama silaha.
Mosri anakabiliwa na kesi pamoja na viongozi wengine wa Kundi la Muslim Brotherhood kwa kuwachochea wafuasi kumuua mwandishi wa habari na waandamanaji wa upinzani wakati wa makabiliano nje ya ikulu ya rais mwaka 2012.
Mawakili wanaomtetea Mosri wanasema kuwa huenda akakabiliwa na hukumu ya kifo. Mamia ya wafuasi wa Kundi la Muslim Brotherhood wamehukumiwa kifo katika mikakati ya kukabiliana na kundi hilo lililopigwa marufuku na rais wa sasa Abdul Fattah al-Sisi.
Kundi la Muslim Brotherhood limemlaumu rais kwa kutumia mahakama kama silaha.

Note: Only a member of this blog may post a comment.