Thursday, March 26, 2015

Anonymous

NEWS ALERT: ASKOFU GWAJIMA MATATANI KWA MADAI YA KUMTUSI PENGO, ATAKIWA KURIPOTI JESHI LA POLISI!

Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamtaka Askofu JOSEPHAT GWAJIMA wa Kanisa la Ufufuo na Uzima afike haraka katika kituo cha Polisi chaKati ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum ya Dar es Salaam kwa mahojianokuhusu tuhuma za kashfa na matusi.

Tumepokea malalamiko ya kukashifiwa na kutukanwa hadharani Mwadhama KaldinariPolycarp Pengo ambaye ni kiongozi wa Kanisa Katoliki nchini Tanzania. Kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii kama vile WhatsApp na mingineyo kuna sautiiliyorekodiwa (audio) na picha za video (Video Clip) zikimuonyesha Askofu
Gwajima akimkashfu na kumtukana kwa maneno makali Kaldinari Pengo katika hali ambayo pia imewaudhi watu wengine.


Baada ya tukio hilo juhudi mbalimbali zimekuwa zikifanyika katika hali ya kawaida ili kumpata Askofu Gwajima bila mafanikio na hivyo yeye mwenyewe sasa anatakiwa aende akaripoti haraka kwa Mkuu wa Upelelezi wa Kanda Maalum ya Dar es Salaam bila kukosa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.