Monday, March 16, 2015

Anonymous

MITANDAO YA KIJAMII INAYOTUMIKA VIBAYA KUFUNGWA TANZANIA?! TAMKO LA TCRA HILI HAPA

Baada ya Gazeti Moja Kubwa Kuandika kuwa TCRA ipo Mbioni kufunga Mitandao ya Kijamii inayotumika Vibaya ..TCRA wameibuka na Kusema :

'TCRA haina mpango huo na haikusudii kufanya hivyo na haina Mamlaka ya kufungia mtandao uliosajiliwa nje ya Tanzania.

Tumejikita zaidi kutoa elimu kwa umma juu ya matumizi mazuri ya mawasiliano. Wanaotumia mitandao vibaya ni wachache kuliko wanaotumia vizuri.

Habari hii sio kweli hakuna wakati wowote ambapo yeyote katika mkutano huo alizungumzia kufunga mitandao ya kijamii. Kwa mtu anayefahamu teknolojia anaelewa madhara na hasara ya kufanya hivyo.

Waandishi wa habari wanaaswa kuwa makini wanapoandika habari kuepusha kutoa habari ambazo sio sahihi na zinazoweza kuleta mtafaruku kwa jamii'

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.