Mapenzi
ya mashabiki kwa mastaa mbalimbali huwa yanaonekana kwa njia nyingi,
wengine wanavaa kama mastaa hao, wengine wananyoa, au kusuka.. Yani
shabibiki anafanya chochote ili kuonyesha jinsi ambavyo ana mapenzi na
staa huyo.
Huyu ni shabiki wa nguvu wa Rihanna, ameamua kujichora tattoo 14 mwilini mwake kutokana na mapenzi aliyonayo kwa mwanamuziki huyo.
Sara Ridge ni shabiki huyo raia wa Afrika Kusini, ana tattoo saba zenye sura ya Rihanna katika mwili wake na ametumia zaidi ya paundi 2,000 kama gharama ya kujichora, katumia saa zaidi ya 48 mpaka zoezi lote limekamilika.
Mbali na picha hizo sehemu nyingine amechora maandishi ya mashairi ya nyimbo za staa huyo.
Mama yake Sarah alimkataza mwanae kuchora tattoo hizo akimsihi kwamba huenda siku moja akajutia kufanya hivyo.
“Marafiki
zangu na ndugu zangu hawakukubaliana na maamuzi yangu lakini kwa kuwa
mwenyewe nilitaka kufanya hivyo, sikupenda kusikiliza ushauri wa mtu
yoyote… siwezi kuja kujutia“– Sara.

Note: Only a member of this blog may post a comment.