Wednesday, March 11, 2015

Anonymous

[7 PICHAZ] SHANGINGI LA SERIKALI LAPARAMIA UKUTA WA SHULE JIJINI DAR

Gari ya Serikali aina ya Toyota Land Cruser yenye namba za Usajili STK 7278, ikiwa imeparamia ukuta wa Shule ya msingi Al Muntazir iliyopo kwenye makutano ya barabara ya Sea View na Barack Obama Drive jijini Dar es salaam mara baada ya dereva wake (jina kapuni) kushindwa kulimudu gari hilo pale alipochomekewa na gari nyingine ambayo iliingia mitini. 
Ajali hii imetokea jana jioni wakati gari hilo likiwa linatokea mjini kuelekea Palm Beach hakuna aliyejeruhiwa katika ajali hiyo.

Wafanyakazi wa "Break Down" wakiangalia namna ya kuichomoa gari hiyo iliyoparamia ukuta wa Shule ya msingi Al Muntazir iliyopo kwenye makutano ya barabara ya Sea View na Barack Obama Drive,jijini Dar es salaam leo.
CHANZO MTAA KWA MTAA BLOG


Hivi ndivyo ionekanavyo gari hiyo mara baada ya kuchomolewa kwenye ukuta huo.

Mashuhuda wakitazama gari hiyo.

Gari hiyo ikivutwa na "Break Down" mara baada ya kuchomolewa ukutani

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.