Inspekta Puyo Nzalayaimis akisoma tamko mbele ya waandishi wa habari (hawako pichani).
JESHI la Zimamoto na Uokoaji nchini limesema ukosefu wa taarifa
kamili kuhusu eneo la ajali ya moto ambayo ilitokea Februari 7 mwaka huu
na kuua watu sita wa familia moja katika Kata ya Kipawa, Mtaa wa
Kipunguni ‘A’ jijini Dar ndiyo ulisababisha jeshi hilo kuchelewa kufika
katika eneo hilo na kufanya uokoaji. Hayo yalisemwa na msemaji wa jeshi hilo, Inspekta Puyo Nzalayaimis leo jijini kuhusiana na nyumba ya David Mpira ambaye naye alifariki katika tukio hilo ambapo nyumba yake ilianza kuungua usiku ambapo jeshi lake lilifika saa 12 alfajiri na kukuta nyumba yote imeteketea na moto kuwaua watu wote waliokuwa ndani.
Ofisa huyo aliwataka wananchi kutoa taarifa mapema ya tukio husika kwa kupiga namba ya dharura 114 ili kuliwezesha jeshi kufika kwa muda mwafaka, na kwa mtu anayetoa taarifa kuhakikisha anatoa maelezo ya kina ya eneo la tukio na jinsi ya kufika sehemu husika pasipo kuzima simu yake ya mkononi.
Pia alitoa wito kwa wananchi kuelewa manufaa ya uwekaji wa vifaa vya kuzimia moto katika majumba yao ili kupambana na majanga ya moto unapotokea.
JIUNGE
NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU
UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142.ASANTE NA KARIBU
TENA!
(HABARI/PICHA : DENIS MTIMA/GPL)

Note: Only a member of this blog may post a comment.