Friday, February 13, 2015

Anonymous

PICHAZ: LIPUMBA AWASIHI JUVICUF WASIANDAMANE, WAKUBALIANA NAYE

Polisi wakiwa wamejiimarisha kuzuia maandamano ya Vijana wa CUF eneo la Buguruni.
Wananchi wakijadiliana kuhusu tukio hilo.
MWENYEKITI wa Taifa wa Chama cha Wananchi (CUF)  Profesa Ibrahim Lipumba leo amewasihi Jumuiya ya Vijana wa CUF(JUVICUF) kusitisha maandamano kama jeshi la polisi lilivyoagiza . 

Akizungumza leo katika ofisi za chama hicho zilizopo Buguruni, jijini Dar e s Salaam,  amesema kuwa vijana hao waache kuandamana kwa sababu kunaweza kutokea madhara makubwa ikiwa ni pamoja na  kupigwa risasi, vifo na kadhalika. 

Alisisitiza waache kuandamana ingawa dhamira yao  ya kuitaka  Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) iongeze siku za uandikishwaji wa upigaji kura  kutoka siku saba hadi 14 ina mantiki kwa Watanzania wote.  

JIVICUF walikuwa waandamane kusisitiza, miongoni mwa mambo mengine, kuhusu uvunjwaji  wa haki za binadamu nchini na dosari za uandikishaji wapiga kura. 
JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142. 
ASANTE NA KARIBU TENA!
(Habari/Picha: Gabriel  Ng’osha/GPL)

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.