Saturday, February 14, 2015

Anonymous

MSHTUKO! MAMA KANUMBA ANA LAANA!

Stori: Laurent Samatta/Risasi  
BABA wa marehemu Steven Kanumba, Charles Kanumba amemchana mzazi mwenzake, Flora Mtegoa kuwa anateswa na laana na ndiyo maana hafanikiwi.
Baba wa marehemu Steven Kanumba, Charles Kanumba.
Mzee huyo alisema mama Kanumba ameshindwa kufanikiwa katika mambo mengi likiwemo suala la kuendeleza ofisi ya marehemu kutokana na kushindwa kumshirikisha yeye kama baba na ndiyo maana amepata laana.
“Tatizo ni papara ya mwezangu ya kutaka mali ndiyo mambo yanayotokea na kamwe hataweza kufanikiwa kwa sababu baraka za mtoto zinatoka kwa mama na baba na hiyo laana itazidi kummaliza sababu hakunishirikisha,” alisema.

Mama Kanumba Flora Mtegoa.
Alipotafutwa mama Kanumba kuhusiana tuhuma hizo, alisema:
“Huyo mzee yeye ndiyo ana laana, nimeshamzoea, hana jipya amekalia majungu. Mimi sina laana, nakaa kwenye nyumba ya maana na si kama yeye anayeishi kwenye nyumba ya udongo.”

JIUNGE NASI FACEBOOK > >>BONYEZA HAPA.KAMA KUNA TATIZO AU UNA PICHA ZA MATUKIO TUTUMIE WHATSAPP +255 712 919 142. 
ASANTE NA KARIBU TENA!

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.