Wednesday, December 21, 2016

Unknown

Mshambuliaji Romelu Lukaku kuweka rekodi mpya Everton!

Mshambuliaji wa klabu ya Everton Romelu Lukaku anatarajia kupewa mkataba mpya na klabu hiyo ya Everton ambao atakuwa akilipwa pauni 100,000.

Kiwango hicho cha malipo, kitamfanya Lukaku ambaye ni raia wa Ubelgiji ataweka rekodi ya kuwa mchezaji wa kwanza wa Everton kulipwa kiasi hicho kwa wiki.

Everton ambayo uwanja wake wa nyumbani ni Goodison Park ambao upo jijini Liverpool, haijawahi kutoa pauni 100,000 kwa mchezaji yoyote.

Lukaku ambaye alijiunga na Everton Juni, 2019 akitokea Chelsea na imeelezwa wakala wake Mino Raiola amekuwa katika mazungumzo mazito na uongozi wa Everton.

Majira ya joto, nusura Lukaku arejee tena Chelsea lakini suala hilo lilishindikana baada ya mwekezaji mpya wa Everton, Farhad Moshiri kusisitiza anataka bado aendelee kubaki.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.