Yawezekana wewe ni mmoja wa wanaotamani kwenda kupumzika kwenye visiwa vya marashi ya karafuu Zanzibar kwani wengi hupenda kufanya utalii visiwani humo kutokana na mengi mazuri yanayopatikana ndani ya visiwa hivyo.
Amri hiyo iliyotolewa na kiongozi huyo imemgusa Mwenyekiti wa Kamati za Baa Zanzibar Hussein Ali Kimti na kusema kitendo cha kupunguza muda wa saa zao za kazi kutapelekea ugumu mkubwa wa maisha yao ya kila siku kwani ni wazi kipato chao kitaporomoka kwa kasi.
Lakini pia Mwanasheria wa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Vyakula na vinywaji Zanzibar, Hassan Cornel amesema agizo lililotolewa na mkuu huyo wa mkoa ni zito kwa wafanyabiasahra hao kwani wamekuwa wakilipa kodi hivyo amemtaka kuweka mikakati mizuri ili kuendana na mazingira ya kodi zao.
Note: Only a member of this blog may post a comment.