Thursday, October 6, 2016

Unknown

Waziri Ndalichako awatimua Chuo walimu wa mafunzo waliompiga mwanafunzi shule ya Kutwa Mbeya

Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi Profesa Joyce Ndalichako amewafukuza chuo walimu wanafunzi watatu kwa tuhuma za kumpiga mwanafunzi Sebastian Singuli wa Shule ya Sekondari Mbeya Day. Profesa Ndalichako amesema kwa mujibu taratibu za vyuo vikuu kitendo kilichofanywa na wanafunzi hao ni kosa la jinai na hawawezi kuendelea na taaluma ya ualimu kwa sababu wamekosa sifa ya kuwa walimu.

Mpaka sasa Mkuu wa Shule na baadhi ya walimu wamefikishwa katika kituo cha polisi kwa mahojiano kuhusiana na tukio hilo.
Aidha Prof Ndalichako ameelezea kusikitishwa kwake pamoja kuchukizwa na kitendo hicho ambacho amesema si cha kawaida na hakiwezi kufumbiwa macho katika jamii. 
– TBC

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.