Msanii wa filamu Daudi Michael Tairo, anayefahamika zaidi kwa jina la Duma ndani ya tamthilia ya Siri ya Mtungi, amefunguka na kueleza jinsi tamthilia hiyo ilivyompatia mashavu ndani na nje ya nchi.
“Tamthilia ya ‘Siri ya Mtungi’ imenifungulia milango mingi sana na ndio tamthilia ambayo naiheshimu kwa kunifungulia milango ya kitaifa na kimataifa,” alisema Duma. “Ilinifanya nikapata deal Kenya na kuigiza kwenye tamthilia ambayo tayari imesharuka, kwa hiyo naweza kusema ni tamthilia ambayo imenipatia jina ambalo kwa sasa ndo nalitumia kama brand na hakuna mtu yeyote ndani ya bongo movie ambaye analitumia,”
Pia mwigizaji huyo amesema tasnia ya filamu kwa sasa inaushindani mkubwa hali ambayo inawafanya wasanii kuandaa kazi nzuri ili kuweza kufanya vizuri.
Mwigizaji huyo kwa sasa anafanya vizuri na filamu yake mpya iitwayo ‘Mchongo sio’.
Note: Only a member of this blog may post a comment.