Thursday, September 29, 2016

Unknown

Donald Trump adaiwa kupoteza $800m kwa kipindi cha mwaka mmoja!

Kama akikosa urais wa Marekani, Donald Trump anasababu chungu mzima za kujilaumu kutokana na kutumia fedha nyingi huku jarida la Forbes likiripoti kuwa mfanyabiashara huyo amepoteza zaidi ya $800 milioni kwa kipindi cha mwaka mmoja.

Jarida hilo limedai hali hiyo imetokana na kudorora kwa soko la nyumba na ardhi nchini Marekani huku kati ya majumba 28 ambayo yalichunguzwa na Forbes, 18 yalishuka thamani likiwemo jengo maarufu la Trump Tower linalopatikana Manhattan pamoja na vilabu vyake vya Mar-a-Lago vilivyopo Palm Beach, Florida.

Hata hivyo jengo lake la pili kwa urefu la San Francisco limedaiwa kupanda thamani kati ya majengo saba yaliyotangazwa kupanda thamani.

Mpaka sasa inakadiriwa mgombea huyo wa urais wa chama cha Republican ameshatumia zaidi ya kiasi cha $55 milioni kutoka mfukoni kwake kwenye kampeni hizo.

Forbes wanakadiria kwamba matamshi yake dhidi ya wahamiaji wa Mexico yalimgharimu $100m kupitia mikataba aliyopoteza kwenye mashirika makubwa kama vile NBC Universal, Univision na Macy’s.

Lakini Forbes wanadai kuwa utajiri wa Trump ni dola bilioni 3.7 huku vyanzo vingine kama Bloomberg kimedai kuwa ana utajiri wa $3bn nao Fortune wanasema ana $3.9bn.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.