Ndugu wakiwa katika Hospitali ya Muhimbili.
DAR ES SALAAM: Ni tukio la ajabu! Simulizi vinywani
mwa wakazi wa Jiji la Dar ni lile tukio la kusikitisha la mwili wa
marehemu kukabidhiwa watu wasio ndugu na kwenda kuuzika kwao huku ndugu
wakiambulia patupu licha ya kufika mochwari na jeneza, AMANI lina mzigo
wote.
Tukio hilo la aina yake lilijiri Aprili 11, mwaka huu kwenye
Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) jijini Dar ambapo familia ya Theodory
Chivumile wa Ukonga- Gerezani kuukosa mwili wa Janeth Mtonga Theodory
(52) kwa kuambiwa kuwa, ulichukuliwa na familia nyingine na kwenda
kuuzika, Usangi mkoani Kilimanjaro
TWENDE HATUA KWA HATUA
Kwa mujibu wa mtoto wa marehemu, Raymond Theodory siku hiyo familia walipanga kufanya mazishi maana mpendwa wao alifariki dunia Ijumaa ya Aprili 8, mwaka huu kwenye hospitali hiyo.
“Lakini katika hali ya kushangaza huku waombolezaji wakiwa nyumbani wakisubiri mwili ili kuuaga, tulifika Muhimbuli tukaambiwa mwili wa mama umechukuliwa na ndugu zake.”
Kwa mujibu wa mtoto wa marehemu, Raymond Theodory siku hiyo familia walipanga kufanya mazishi maana mpendwa wao alifariki dunia Ijumaa ya Aprili 8, mwaka huu kwenye hospitali hiyo.
“Lakini katika hali ya kushangaza huku waombolezaji wakiwa nyumbani wakisubiri mwili ili kuuaga, tulifika Muhimbuli tukaambiwa mwili wa mama umechukuliwa na ndugu zake.”
Jeneza likiwa tupu ndani ya gari.
MSHANGAO MKUBWA
“Tulishangaa sana! Ndugu zake akina nani wakati ndiyo sisi! Wakasema ndugu waliouchukua mwili wameusafirisha Kilimanjaro kwa mazishi, tukazidi kuchanganyikiwa,” alisema mtoto huyo.
“Tulishangaa sana! Ndugu zake akina nani wakati ndiyo sisi! Wakasema ndugu waliouchukua mwili wameusafirisha Kilimanjaro kwa mazishi, tukazidi kuchanganyikiwa,” alisema mtoto huyo.
MSIMAMO WA FAMILIA
Aliendelea: “Bado hili tukio halituingii akilini, sidhani kama wale
ndugu walishindwa kuutambua mwili wa marehemu wao na kumchukua marehemu
wetu. Ninafikiri ni uzembe tu uliofanyika maana marehemu wote huwa
wanawekewa majina, wetu alikuwa anaitwa Janeth wao Amina, hapo mtu
anaweza kuchanganya vipi? Tunaomba suala hili lichunguzwe.”
NDUGU WENGINE
Gazeti hili pia lilifanikiwa kuzungumza na mume wa marehemu aitwaye
Theodory Chivumile ambaye hakupenda kupigwa picha kutokana na sababu
binafsi, naye alionesha kushangazwa na tukio hilo lakini alisisitiza
kwamba, wao kama familia hawahusiki kwa lolote na kilichotokea, kikubwa
wanamtaka marehemu wao.
WIFI WA MAREHEMU
Luciana Saulenda ni wifi wa marehemu ambaye alionesha masikitiko yake makubwa na kusema haya:
“Sisi ni Wakristo, kwa hiyo marehemu wetu amekwenda kuzikwa kwa taratibu zingine na tutalazimika kumzika tena kwa taratibu zetu baada ya kufukuliwa. Kwa kweli si sahihi kilichofanyika. Tumeumia sana.”
Luciana Saulenda ni wifi wa marehemu ambaye alionesha masikitiko yake makubwa na kusema haya:
“Sisi ni Wakristo, kwa hiyo marehemu wetu amekwenda kuzikwa kwa taratibu zingine na tutalazimika kumzika tena kwa taratibu zetu baada ya kufukuliwa. Kwa kweli si sahihi kilichofanyika. Tumeumia sana.”
MUHIMBILI WANASEMAJE?
Kwa upande wa uongozi wa Muhimbili walisema ndugu waliofanya makosa ni
wale walioanza kwenda kuuchukua mwili wa marehemu ambao si wa kwao na
kwenda kuuzika bila kuuhakiki kwanza.
“Ile familia nyingine ni Waislam na ndiyo walisababisha haya yote maana walimchukua marehemu bila kumkagua kuwa ni wa kwao na kwenda kumzika. Nadhani ni kwa sababu ya utaratibu wao.
“Ile familia nyingine ni Waislam na ndiyo walisababisha haya yote maana walimchukua marehemu bila kumkagua kuwa ni wa kwao na kwenda kumzika. Nadhani ni kwa sababu ya utaratibu wao.
“Lakini tumeshawasiliana nao, leo (Jumatatu) gari letu limekwenda
mkoani Kilimanjaro, kesho (Jumanne) tutamrudisha marehemu na kumkabidhi
kwa ndugu zake kwa ajili ya taratibu zingine za mazishi,” alisema Dk.
Mosha mmoja wa viongozi wa kitengo cha mochwari hospitalini hapo.
Marehemu Janeth enzi za uhai wake.
Hadi tunakwenda mitamboni, ndugu wa marehemu Janeth walidai
wanasubiri mpaka wakabidhiwe ndugu yao ndipo wafanye taratibu zingine za
mazishi huku msibani nyumbani, meza ya kuweka jeneza wakati wa kuuaga
mwili na mapambo mengine vikiendelea kuwepo.
Kuna taarifa kwamba, jeneza walilokwenda nalo kwa ajili ya mwili,
lililala kwenye gari na muda mwingi ndugu hao walikuwa wakipiga simu kwa
wahusika wa Muhimbili kuulizia wa Kilimanjaro wamefikia wapi katika
kuurudisha mwili wa ndugu yao, Dar.
Note: Only a member of this blog may post a comment.