Wednesday, April 13, 2016

Anonymous

TEKNO Ajizawadia Benz Baada ya Kupata Mtoto

11055595_836375646419073_35542390_n
Staa wa muziki kutoka Naija, Tekno Miles.
STAA wa muziki kutoka Naija, Tekno Miles kwa sasa ana furaha isiyoelezeka baada ya kubahatika kupata mtoto na kujizawadia gari aina ya Mercedes Benz CLS 550.
image (3) 
Kichanga cha Tekno Miles.
Staa huyo ambaye yupo kwenye Lebo ya Triple MG, ameingia kwenye kundi la wasanii wenye watoto baada ya hivi karibuni kuripotiwa kutoka na wasichana kadhaa nchini Afrika.
Hata hivyo kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii alitupia picha ya mtoto huyo ambapo hakuweka wazi jinsia wala mama wa mtoto.
image (4)Mercedes Benz CLS 550 alilojizawadia Tecno baada ya kupata mtoto.
Tusubiri kujua zaidi kama ni mtoto wake kweli ama ‘sound’ za mjini kutokana na mastaa wengi nchini Nigeria kudanganya kuwa na watoto kupitia mitandao ya kijamii.
(Imeandaliwa na Andrew Carlos/GPL)

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.