Staa wa muziki kutoka Naija, Tekno Miles.
STAA wa muziki kutoka Naija, Tekno Miles kwa sasa
ana furaha isiyoelezeka baada ya kubahatika kupata mtoto na kujizawadia
gari aina ya Mercedes Benz CLS 550.
Kichanga cha Tekno Miles.
Staa huyo ambaye yupo kwenye Lebo ya Triple MG, ameingia kwenye kundi
la wasanii wenye watoto baada ya hivi karibuni kuripotiwa kutoka na
wasichana kadhaa nchini Afrika.
Hata hivyo kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii alitupia picha
ya mtoto huyo ambapo hakuweka wazi jinsia wala mama wa mtoto.
Tusubiri kujua zaidi kama ni mtoto wake kweli ama ‘sound’ za mjini
kutokana na mastaa wengi nchini Nigeria kudanganya kuwa na watoto
kupitia mitandao ya kijamii.
(Imeandaliwa na Andrew Carlos/GPL)

Note: Only a member of this blog may post a comment.