Sunday, April 3, 2016

Anonymous

Ndugu wa Marehemu Sajuki Afungukia Talaka ya TALAKA Aliyopewa na Mheshimiwa Mbunge

KUTOKANA na madai ya kupewa talaka na mumewe Sadifa Juma, ndugu wa aliyekuwa mume wa Wastara Juma, marehemu Sadick Kilowoko ‘Sajuki’, Mohamed Kingochi ‘Mdidi’ amefunguka kuwa ameumizwa na suala hilo kwani walitegemea ndiyo amepata mtu wa kumpa faraja.

Akipiga stori na paparazi wetu, Mdidi alisema wakati Wastara anaolewa walihuzunika ila siyo kwamba hawakutaka aolewe bali ni kutokana na mazoea kwamba watakosa kuwa naye karibu.
“Madai ya talaka ya Wastara yameniumiza sana kwani tulikuwa tunatatarjia akishakaa vizuri kwenye ndoa tuendeleze Kampuni ya WAJEY lakini tangu ameolewa, mambo ni vululuvululu na hili la talaka nalo ndiyo linazidi kutuumiza,” alisema Mdidi.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.