Wednesday, April 13, 2016

Anonymous

Kifo Cha NDANDA Kosovo ...Mke Asimulia Mazito

MKE WA NDANDA (2)
Mke wa Ndanda Kosovo ‘Kichaa’, aitwaye, Loving Chitoto.
NA Richard Bukos, RISASI mchanganyiko DAR ES SALAAM: Wakati mwanamuziki nyota aliyefariki mwishoni mwa wiki iliyopita, Ndanda Kosovo ‘Kichaa’ anatarajiwa kuzikwa leo katika Makaburi ya Kinondoni jijini Dar, mkewe aitwaye Loving Chitoto, amesimulia mazito juu ya mumewe. 

Akizungumza na paparazi wetu nyumbani kwake Kionondoni-Hananasif, Chitoto alikumbusha kuwa alikutana na Ndanda mwaka 1999, kabla ya mwaka 2000 kumuimba katika wimbo wake wa Prison maarufu kama Wajelajela na kabla ya kutimkia Stono Musica. 

Akielezea mapenzi yao, Chitoto alisema kama Mungu angewajaalia basi wangekuwa na watoto wanne hivi sasa, lakini wamebakia na mtoto mmoja aitwae Okito ambaye Septemba, mwaka huu anatarajia kutimiza miaka mitatu.
12934847_1064063696984266_1609999490_n 
Ndanda Kosovo enzi za uhai wake.
Akifafanua, Chitoto alisema awali mwanzoni mwa mapenzi yao, walibahatika kupata mtoto aliyeitwa Patrick lakini alifariki dunia.
Baada ya hapo alipata ujauzito mwingine na kufanikiwa kupata watoto mapacha, lakini nao walifariki dunia muda mfupi baada ya kuzaliwa.

Aliendelea kusema licha ya mikasa hiyo hawakukata tamaa, waliendelea na mapenzi yao mpaka alipopata ujauzito na kumpata Okito ambaye Mungu amempa uzima hadi sasa.
“Ukweli siwezi kumsahau baba watoto wangu Ndanda, tumetoka mbali na tulitarajia kufika mbali zaidi, lakini kazi ya Mungu haiingiliwi,” alisema Chitoto huku akijifuta machozi.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Mazishi ya mwanamuziki huyo, King Dodoo marehemu anatarajiwa kuzikwa leo Jumatano kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar ambapo maandalizi yamefanyika kwenye nyumba ya Ubalozi wa Congo DRC iliyopo Kinondoni-Hananasif jijini.

Dodoo alisema wameamua kumzika marehemu hapa nchini kufuatia wosia wake alioutoa mbele ya Waziri wa Habari, Vijana, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye wakati akizungumza na wanamuziki wa dansi katika Ukumbi wa Vijana Kinondoni mwezi uliopita.

Katika kikao hicho Ndanda alisimama na kusema endapo akifa basi maiti yake izikwe hapa Tanzania kwa kuwa ndipo mahali alipopatia mafanikio makubwa ya kimuziki na anahisi ndiyo sehemu ambayo atazikwa na watu wengi kuliko Lubumbashi alikozaliwa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.