Monday, April 11, 2016

Anonymous

Huu Ndio Ujio Mpya wa Mtangazaji Mahiri GADNER G HABASH Ndani ya Clouds FM Leo Hii Tarehe 11

Msimu Mpya Clouds FM
Mwezi huu umekuwa wa mapambano makubwa kati ya vituo vya redio viwili jijini Dar es Salaam, Clouds FM na EFM.

EFM walibomoa kipindi cha Power Breakfast kwa kuwachukua Gerald Hando, Paul James na mtayarishaji wa kipindi hicho, Abel Onesmo huku Clouds FM wakikibomoa kipindi cha Ubaoni cha EFM kwa kumchukua mtangazaji wake wa zamani, Gardener G Habash.

Gardener aka Captain anaanza kazi rasmi Jumatatu hii kwenye msimu mpya wa kituo hicho kwa kuendelea kukiendesha kipindi chake cha zamani, Jahazi.

Mtangazaji huyo anadaiwa kupewa mshahara mnono unaoweza kumfanya kuwa mtangazaji anayelipwa fedha nyingi zaidi kuliko wote Tanzania. Kwanza miongoni mwa vitu alivyopewa ili kurejea tena CMG ni gari aina ya Land Rover Discovery na mashavu mengine mengi.

Kwa upande wa EFM kuna kila dalili kuwa kipindi chao cha asubuhi kitapata nguvu mpya kuanzia wiki hii. Haijulikani ni watu wapi Clouds FM wamewachukua kuziba pengo lililoachwa kwenye Power Breakfast.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.