Biashara ya ngono imezidi kushamiri Duniani siku baada ya siku, hata hapa nchini mtembezi imeshuhudia serikali ikitoa matamko mbalimbali dhidi ya Biashara hiyo.
Chini ya sheria hiyo mpya, watu watakaokutwa wakilipia huduma hiyo wataadhibiwa kwa kulipa dola 1,700.
Mmoja wa mbunge anayeunga mkono sheria hiyo ameitetea na kusema kuwa inalengo la kuhamasisha watu kujiondoa katika biashara hiyo.
Hata hivyo kundi dogo la makahaba waliandamana nje ya bunge wakipinga sheria hiyo kwa madai kuwa wapewe uhuru wa kujilinda wenyewe na si kukatazwa kufanya biashara hiyo.
Ni vyema serikali ya jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikaiga mfano huo wa nchi ya Ufaransa na kuweka mikakati maalum itakayo pelekea watu kujiajiri.
Note: Only a member of this blog may post a comment.