Monday, March 14, 2016

Anonymous

Kanye West Ameingia Tena Kwenye Headline!

kanye-west-facts-gi
Kanye West.
HABARI njema ikufikie popote ulipo ewe shabiki wa Kanye West na tasnia nzima ya muziki wa Hip Hop. Kutokana na kukaa kimya na kutokuachia albamu yeyote kwamiaka miwili 2014 na 2015 kitu ambacho haikuwa kawaida yake. Rapa maarufu duniani ambaye hivi karibuni aliachia albamu yake inayoitwa ‘The Life of Pablo’, Kanye West mwishoni mwa wiki jana aliibuka na kusema anatarajia kuachia albamu tatu kwa mwaka huu kuanzia sasa.
kanye-west-announces-swish-release-date
Rapa huyo alithibitisha kauli yake hiyo alipoandika kwenye akaunti yake ya Twitter ataachia albamu tatu kwa mwaka huu wa 2016, pia aliongeza kuwa atatengeza matoleo sita ya viatu vyake vyenye lebo ya Yeezy kwa mwaka. 
No more fashion calendar... I'm going Mad Max... 6 collections a year...3 albums a year
West aliachia albamu yake ya The Life of Pablo mwezi uliopita, ambayo mapaka sasa inaendelea kufanya vizuri kwenye vituo mbalimbali vya radio na televisheni duniani.west amesema kuwa hakuna albamu yake hata moja kati ya hizo amabyo itakuwa kwenye mfumo wa CD.
Miaka mitatu iliyopita kabla ya Pablo, West aliachia albamu yake ya Yeezus. Hiyo ni baada ya 2010 alipoachia My Beautiful Dark Twisted Fantasy. 2004 aliachia The College Dropout na kukaa kimya mpaka mwezi jana alipoachia The Life of Pablo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.